0
Your Cart
No products in the cart.
Sabina Ntobi

Malindi Estate waandaa matembezi kuhimiza watu kushiriki Sensa

Na Sabina Ntobi Uongozi wa Serikali ya mtaa Malindi Estate, Kinondon Jijini Dar es Salaam, umeandaa matembezi ya hiari kwa ajili ya kuhimiza wananchi wa maeneo hayo kushiriki kikamilifu kwenye zoeli la Sensa ya Watu na Makazi. Mwenyekiti wa mtaa huo,Clement Mshana amesema matembezi hayo yatafanyika Agosti 20 mwaka huu, kuanzia saa kumi na moja alfajiri na yataanzia eneo zinapojengwa ofisi za Serikali ya mtaa, barabara ya Flamingo na Obama,Mbweni na kuishia Uwanja wa Ubungo,Mbweni. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Mtaa ,mgeni rasmi wa shughuli hiyo atarajia kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni. Akifafanua zaidi, Mshana amesema dhumuni la hayo matembezi ni kutoa elimu kwa wananchi juu ya masuala mbalimbali yanayohusiana na sensa. Aidha,amesema baada ya matembezi hayo, wananchi watapewa ufafanuzi kuhusu viambatanisho vinavyohitajika wakati wa sensa na maswali muhimu yatakayoulizwa wakati wa zoezi hilo ili kuwaandaa wananchi na ili kuzuia kupoteza muda. Zoezi la sensa ya watu na makazi litafanyika Agosti 23, 2022 nchini kote kwa lengo kufahamu idadi kamili ya watu na kuweka bajeti inayotosha kwa ajili ya wananchi wote na maendeleo yao.

Add a Comment

Your email address will not be published.

All Categories

Get Free Consultations

SPECIAL ADVISORS
Quis autem vel eum iure repreh ende